Pages

Friday, February 22, 2013

NIDHAMU NI NINI?

Nidhamu ni uwezo wa kufanya mambo / vitu fulani pasipo kufuata hisia (kinyume na ulivyozoea). Baada ya kutoa tafsiri hiyo fupi iliyobeba shehena ya maarifa na uwezo wa kubadilisha maisha ya mtu binafsi, James alizungumzia na kufafanua maeneo nane (8) ambayo yanahitaji nadhamu kali.


UNATAKIWA UWE NA NIDHAMU KALI KATIKA MAENEO NANE (8).

1. Eneo la kujiwekea malengo binafsi kila mwaka.

* Kujiwekea fursa/possibilities; mfano. mwaka huu nitafanya a, b, c... ukiendelea zaidi utatoka kwenye mwaka itakuwa malengo ya mwezi hatimaye kila siku.
* Mtu mwenye malengo anajua kule anakoenda, mtu asiye na malengo hawezi kwenda na hajui anakokwenda.
* Malengo yanakupa uwezo wa kudhibiti mabadiliko ya maisha katika dunia.
* Malengo yatakupa FOCUS.
* Siri moja ya mafanikio duniani ni kuwa na FOCUS.
* Malengo yatakufanya uwe namba moja (1), Mafanikio yanakuja kwa kufanya yale uliyojiwekea kuyafanya.


2. Nidhamu ya kufikiri vizuri / clear thinking.

* Ni uwezo wa kufikiri vizuri bila bughudha.
Hapa ananukuu msemo mmoja usemao; Those who cannot go within cannot go without.
* Mali ni uwezo wa mtu kufikiri vizuri / uwezo wa kutumia akili vizuri/zaidi.
Nukuu chanya: 'TATIZO SIO UDONGO TULIO NAO BALI UBONGO TULIO NAO'
* Njia rahisi ya kufikiria vizuri ni kuuzoeza ubongo kufikiri.

3. Nidhamu ya kutunza muda / time management.

- Tatizo tulilo nalo ni kutokutunza muda.
* Maisha ya mtu yeyote yanawakilishwa na kitu kidogo kinachoitwa muda, ukipoteza muda unapoteza maisha yako.
* Kimsingi maisha yako ni muda wako, na muda wako ni maisha yako. Jaribu kujitathmini je! kila baada ya dakika 15 umefanya nini. Usijipe mwanya, usikubali kuchelewa.

4. Nidhamu ya kufanya kazi kwa bidii / deligent / hard working.

* Hakuna sehemu nzuri ya kufanikiwa kama Tanzania kwa sababu watu wengi ni wavivu, watu wengi sio wabunifu (wana-copy na ku-paste).
* Ukifanya kazi kwa masaa ya kawaida utakuwa na maisha ya kawaida, ukifanya kazi kwa masaa yasiyo ya kawaida utakuwa na maisha ya juu zaidi / yasiyo ya kawaida.
* Kama unapenda starehe, fanya kazi kwa nguvu zaidi kuliko mtu yeyote yule.

5. Nidhamu ya kujitunza kiafya.

6. Nidhamu ya kuweka akiba na kuwekeza.

* Kama huwezi kujiwekea akiba mara kwa mara basi uwezo wa ukubwa haupo ndani yako.
* Kuwekeza ni suala la kuwa na miradi.
* Kuwekeza ni kutumia baadhi ya vitu / kitu ulicho nacho kutengeneza mkondo mwingine wa fedha.
* Ukitaka kuwa maskini tumia fedha zote ulizo nazo na ziada kidogo, fedha ambayo huipangilii itaondoka.


7. Nidhamu ya ujasiri / ushujaa / courage.

* Kila mtu duniani anaogopa kitu fulani, Lakini watu ambao wanapanda juu ni wale wanaoishinda hofu / woga. Kuna hofu ya kweli na isiyo ya kweli.
* Jaribu kuzishinda hofu zako, usipozishinda maisha yako yatabaki pale pale.
* Ujasiri unakufanya uwe na uwezo wa kumiliki mambo makubwa / biashara kubwa.

8. Nidhamu ya kujifunza endelevu / continuous learning.

* Kama kuna udhaifu Tanzania ni udhaifu wa kutopenda kujifunza.
* Mtu yeyote ambaye hana tabia ya kusoma ni sawa na mtu ambaye hajui kusoma.
* Nidhamu ya kujifunza ni Elimu binafsi.

Tuesday, January 1, 2013

MAMBO 7 YATAKAYO KUSAIDIA KUTIMIZA NDOTO YAKO




  1. Katika ndoto ulizo nazo, chagua NDOTO moja uanze nayo(ukimbie nayo)
  2. Amini NDOTO yako, uliyonayo siku moja itakuwa kwenye uhalisia
  3. Omba msaada kwa waliokutangulia, mfano NDOTO yako ni kuandika vitabu kuna watu walishaandika vitabu kabla yako,
  4. Kuna nyakati unabidi ubadili mfumo wa maisha yako, ili kuweza kufikia NDOTO yako.
  5. Weka kikomo cha kufanya NDOTO yako, mfano, unataka kuandika kitabu unaweka kuwa utaandika kwa mda gani, labda utaandika kwa miezi 18.
  6. Waambie watu wengine kuhusiana na NDOTO yako uliyonayo, kwasababu unapo tamka neno, kunanguvu, kumbuka hilo, 
  7.  Karika kila Safari kuna vikwazo, usiogope kwa vikwazo vitakavyotokea, na chuga visiwe chanzo cha kutaka kuua NDOTO YAKO