Pages

Saturday, June 9, 2012

Waimbaji ”KWETU PAZURI” Wawasili Dar Leo

 

Sarah Uwera mmoja wa waimbaji wa kundi hilo, walipotembelea nchini mwaka jana

Sarah Uwera mmoja wa waimbaji wa kundi hilo, walipotembelea nchini mwaka jana

Kwaya ya Ambassadors of Christ kutoka jijini Kigali nchini Rwanda imewasili leo Jijini Dar es salaam wakitokea nchini kwao Rwanda, tayari kwa ajili ya kutoa huduma ya uimbaji katika mkutano mkubwa wa kimataifa unaofanyika katika viwanja vya Biafra Kinondoni jijini Dar es salaam.

Kundi la kwanza la kwaya hiyo liliondoka jana kwa njia ya basi kuja jijini, huku kundi la pili ndio limewasili leo mchana.

Hii itakuwa mara ya nne kwa waimbaji hao kufika nchini ambako wamekuwa na mashabiki lukuki, kutokana na uimbaji wao, ambapo safari hii wanatarajia kuwepo kwa wiki nzima jijini Dar es salaam ikiwa maalumu kwa mkutano huo,Pia wanatarajia kuwasili na toleo lao jipya la kanda ambalo baadhi ya nyimbo zimeanza kusikika katika vituo vya radio za injili jijini Dar es salaam.


 

No comments:

Post a Comment